James alibaki pale akiwa na wasiwasi mwingi maana hakujua nini kitafuata baada ya Julieth kufika nyumbani kwao. Tayari mama yake alikuwa amemtafuta na alionekana kuwa na wasiwasi kwa kutomkuta pale kituoni ilhali alijua fika kuwa mwanae alikuwa na James, bila shaka hofu ya mama yake Julieth juu ya uhusiano wao itakuwa imeongezeka. "Mama yake akimuona katika hali hii lazima atajua mimi ndo nimehusika, sijui nini kitafuata", aliwaza James na akili yake ikamwambia pale hapakuwa mahali salama tena kuendelea kuwepo maana Julieth angeweza kumleta mama yake kama angebanwa vizuri. Akaondoka haraka kuelekea kule nyumbani kwa kaka yake ambapo hawakuwa wakipajua.
Kwa namna moja au nyingine James alikuwa akijutia maamuzi yake, matamanio yake yalimuweka katika mazingira mabaya sana wakati ndio kwanza alikuwa anajaribu kuonja maisha mazuri baada ya muda mwingi wa maisha yake kuutumia shule na shamba kule kijijini.
" James naomba leo usiende kazini, lazima mama atakuja kukutafuta maana jana alinitaka kumleta kwako nikadanganya sipajui", ulikuwa ni ujumbe ambao James alikutana nao kwenye simu yake asubuhi alipoamka, ujumbe huu ukitoka kwa Julieth.
Ujumbe ule ulimshitua saa James, moja kwa moja akajua kuwa mambo yalikuwa yamekwisha haribika tayari. Ujumbe ulijieleza vizuri tu kuwa hakutakiwa kufika katika eneo lake la kazi maana mama yake Julieth angeweza kumpata mara moja kama angemtaka. Hivyo akaamua kubaki pale kwa kaka yake ambapo alikuwa na uhakika kuwa hata Julieth tu hakupajua, sembuse huyo mama yake?...
Mida ya saa tatu asubuhi kaka yake James akatoka na mtoto wake ambaye alikuwa anampeleka hospitali kutokana na maumivu ya jino, pia walipanga kupitia mjini kwaajili ya kufanya shopping maana muda wa Peter kurudi shule ulikuwa umekaribia. James akabaki nyumbani na shemeji yake tu ambaye alikuwa wakiendelea na shughuli za usafi wa asubuhi na James akajifungia chumbani mbapo alijaribu kulala lakini usingizi haukuwa karibu, akatoka mpaka sebuleni ambapo alikaa akiangalia luninga, huku akiwa na mawazo tele kichwani mwake. "Shem leo huendi kazini?" Aliuliza Monica baada ya kuwa amepita maraka kadhaa pale sebuleni na akawa anamuona James akiwa katika mkao ambao ulionesha kuwa hakuwa na dalili ya kutoka hivi karibuni ingawa muda wake wa kwenda kazini ulikuwa umetimia. "Hapana leo siendi" alijibu kifupi James, kisha akajifanya kama alikuwa makini sana kufuatilia kilichokuwa kinaendelea kwenye luninga ilhali ukweli ni kuwa alikuwa haoni chochote.
"Kuna nini kwani?" Aliendelea kuhoji Monica ambaye alionekata kutaka maongezi yasiishe kwa sababu zake mwenyewe. "Najisikia uchovu tu leo" alijibu James huku akihitahidi kuyaepuka macho ya Monica ambayo yalikuwa yametua usoni kwake kwa muda mrefu sasa. "Mficha maradhi kifo humuumbua, hebu nambie nini kinakusibu mpenzi" alisema Monica huku akikaa karibu kabisa na James. James akajikuta anashindwa kudanganya zaidi, alitamani kupata mtu wa kuzungumza naye juu ya mkasa wake, hivyo akamuelezea Monica kwa kifupi. "Huyo msichana ana umri gani?" Alihoji Monica baada ya kupewa mkasa ule. "Ana miaka 17" alijibu James. "Mmmmh bado ni mdogo sana, kama wakiamua kwenda mbali itakuwa balaa" alisema Monica. Maneno yale yalikuwa yamoto sana masikioni mwa James, sio kama hakuwa akilijua hilo ila alitamani kupata maneno ya faraja. Monica aligundua kuwa alikuwa ameharibu, hali ya James ilibadilika na kuwa mbaya zaidi toka atamke maneno yale, uoga ulijidhihirisha machoni kwake bila kificho. "Ila hakuna jambo gumu mjini, niachie mimi nitalimaliza hili" alisema Monica, maneno haya angalau yalileta faraja kwa James ingawa hakuona ni kwa namna gani shemeji yake yule angeweza kulimaliza janga lile.
No comments